Sunday, May 13, 2012

Yametimia, Man City bingwa England

Raha ya ushindi
HATIMAYE Manchester City imetwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya England ya EPL baada ya kuifunga QPR mabao 3-2 katika mchezo wa fungadimba huku Manchester United ikishinda lakini City wakijivunia idadi ya mabao ya kufunga.
Ilikuwa Jumapili nyepesi kwa City, kwani walikuwa wakicheza na timu nyepesi ya Queens Park Rangers ambao walifungwa kirahisi. Licha ya Rangers kucheza ikiwa na watu 10, ilipata mabao yake dakika za mwishoni yaliyoipa City heshima.
Ushindi huo uliacha mashabiki kutoa machozi kwa kushindwa kuaamini kilichotokea kwenye Uwanja wa  Etihad, City, iliyokuwa nyuma kwa mabao 2-1 na kushindwa kuipenya ngome ya QPR kwa dakika 51 walibadili upepo na kupata mabao hayo.
Edin Dzeko alifunga bao la kusawazisha kabla ya Sergio Aguero, alifunga na kufanya matokeo kuwa 3-2 kwa shuti la mguu wa kulia na City walianza kushangilia na Manchester kabla ya bao lingine kufungwa.
United, iliyoilaza Sunderland 1-0 na kufungana pointi na City 89, baada ya mpira kumalizika na wachezaji wa United na kocha wao walijipanga kwa ajili ya ubingwa, lakini mambo yalibadilika. Baadaye zilikuja taarifa kuwa Manchester watabakia wa pili kwa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa. Matokeo mengine England:-
Wachezaji wa Man City wakishangilia na kombe lao la ubingwa wa England kutwaa juzi.

Chelsea 2-1 Blackburn
Everton 3-1 Newcastle
Norwich 2-0 Aston Villa
Stoke 2-2 Bolton
Swansea 1-0 Liverpool
Tottenham 2-0 Fulham
West Brom 2-3 Arsenal
Wigan 3-2 Wolves


No comments:

Post a Comment