Wednesday, May 8, 2024

 MAKALLA AWAAMBIA HADEMA; KATIBA MPYA

SIO SAWA NA KUSONGA UGALI


Ripota, ZeNews

Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM, CPA, Amos Makalla amewaambia Chadema kuwa hitaji la Katiba Mpya si sawa na kusonga ugali mara moja umeiva.

Makalla ameyasema hayo leo Mei 8, 2024 kwamba kila mara wapinzani hasa Chadema wamekuwa wakitaka Katiba mpya, na kwamba suala la Katiba ni mchakato.

Amesema Katiba Mpya si sawa na kusonga ugali kwamba unabandika maji, mara yamechemka, unaweka unga, unasonga na ugali tayari.

Makalla amesema Chadema wanapigia kelele Katiba Mpya wakati ndani ya chama chao hakuna demokrasia, na kwamba wangerekebisha katiba yao kwanza ndipo watoke kuzungumzia hili.

Itakumbukwa, Serikali ilitangaza miaka mitatu ya kutoa elimu ya Katiba kabla shughuli ya Katiba haijaanza.

Hata hivyo, Makalla amesema Chadema wangejiangalia kabla ya kudai Katiba kwani hata Mwenyekiti wao, Freeman Mbowe amevunja katiba yao kwa kukaa muda mrefu kama kiongozi wa chama.

 

No comments:

Post a Comment