MAKALLA AWAAMBIA HADEMA; KATIBA MPYA
SIO SAWA NA KUSONGA UGALI
Ripota, ZeNews
Katibu wa Itikadi, Uenezi na
Mafunzo wa CCM, CPA, Amos Makalla amewaambia Chadema kuwa hitaji la Katiba Mpya
si sawa na kusonga ugali mara moja umeiva.
Makalla ameyasema hayo leo Mei 8,
2024 kwamba kila mara wapinzani hasa Chadema wamekuwa wakitaka Katiba mpya, na
kwamba suala la Katiba ni mchakato.
Amesema Katiba Mpya si sawa na
kusonga ugali kwamba unabandika maji, mara yamechemka, unaweka unga, unasonga
na ugali tayari.
Makalla amesema Chadema wanapigia
kelele Katiba Mpya wakati ndani ya chama chao hakuna demokrasia, na kwamba
wangerekebisha katiba yao kwanza ndipo watoke kuzungumzia hili.
Itakumbukwa, Serikali ilitangaza
miaka mitatu ya kutoa elimu ya Katiba kabla shughuli ya Katiba haijaanza.
Hata hivyo, Makalla amesema Chadema
wangejiangalia kabla ya kudai Katiba kwani hata Mwenyekiti wao, Freeman Mbowe
amevunja katiba yao kwa kukaa muda mrefu kama kiongozi wa chama.
No comments:
Post a Comment