![]() |
Wachezaji wa Man. United |
Mpaka sasa, Wolves inashikilia mkia wa ligi hiyo ikiwa na pointi 24 baada ya mechi 36 ikifuatiwa na Blackburn yenye pointi 31.
Timu za Bolton na QPR kila moja zina pointi 34 lakini QPR iko juu ya mstari wa timu tatu zinazotishiwa na kushuka daraja. Pamoja na kujipa matumaini hayo, Aston Villa na Wigan kila moja zina pointi 37 na zinaweza kushuka chini endapo tu Blackburn, Bolton na QPR zitashinda mechi zake na zenyewe kuharibu.
Wakati timu hizo zikishindana mkiani, Manchester City leo itakuwa nyumbani kuialika Manchester United huku kila upande ukijinasibu kushinda mchezo huo.
Makocha wa Pande zote, Roberto Mancini wa Manchester City na Alex Ferguson wa Man United wamekuwa na presha kila mmoja akitamani kushinda mchezo huo.
Mbali na mechi hiyo ya leo, mechi za mwishoni mwa wiki, Everton iliilaza 4-0 Fulham wakati Stoke ikiwa nyumbani, iliivimbia Arsenal na kutoka nayo sare ya 1-1 na Sunderland ilitoka 2-2 na Bolton.
Swansea ilifungana 4-4 na Wolves huku West Brom na Aston Villa zikishindwa kufungana kabla ya Wigan kuibuka na ushindi wa mabao 4-0 dhidi ya Newcastle.
Chelsea iliikamua QPR mabao 6-1 na Tottenham iliilaza Blackburn mabao 2-0 katika mchezo mkali.