Simba wakishangilia bao la kwanza dhidi ya ES Setif |
Simba iliilaza ES Setif ya Algeria katika mchezo mkali uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa na kuhudhuriwa na mashabiki 41,050 licha ya mpambano huo kuonyeshwa live na Clouds TV.
Mabao ya Simba ambayo yamewekwa kimiani na Emmanuel Okwi na Haruna Moshi 'Boban' yataisaidia kwa kiasi kikubwa kuweka uhai kwa timu hiyo ambayo pia haitakiwi kwenda Algiers kwa kujiamini.
Ili kuitoa Simba, inatakiwa kuipiga mabao 3-0 kitu ambacho kwa timu za Waarabu kinawezekana. Kikubwa sasa Simba wajiandae kwa kila aina ya hila za waarabu kwani watafanya kila aina ya kile kinachowezekana kushinda mchezo huo.
Lakini Simba si timu ya kubahatisha, Simba si wageni wa waarabu na tunaamini wanatambua mbinu zao na wanatakiwa kujipanga mapema na wakitaka kuwamaliza ni kusaka bao la mapema.
No comments:
Post a Comment