Saturday, March 10, 2012

Soka ya Tanzania yamsikitisha Matola

Kocha wa timu ya vijana ya Simba na mchezaji wa zamani wa timu hiyo,  Selemani Matola ameelezea kusikitishwa kuona Tanzania ikiendelea kuporomoka viwango vya ubora wa soka kila mwezi.
Kwa mujibu wa viwango vya ubora wa soka vilivyotolewa mwezi huu na Shirikisho la Kimataifa la Soka, FIFA, Tanzania imeporomoka kwa nafasi mbili na sasa iko nafasi ya 141.
Alisema ukiachia wachezaji waliondooka kipindi chao wachezaji walioko sasa kwenye timu yac Taifa wana muda mrefu bila kuleta maendeleo ya kweli kwa kuwa timu zina udhamini hivyo hakuna sababu ya kucheza bila uzalendo.
"Wachezaji wanacheza kama kujifurahisha au kuona ufahari kwamba wameshiriki kwenye michuano fulani,na wana ratiba wanajua kabisa kwamba koch akiita wachezaji ataniita tu lazima kwa kuwa ni wale wale kila siku hawabadiliki,na wanachofanya hakuna," alisema Matola.
Aliongeza kuwa ilitimu ipande badala ya kushuka ni vema wahusika wakaangalia tatizo ambalo kwa ktazamo wake ni kuwatumia wachezaji wakongwe kila siku bila kuwaandaa vijana ambao wataokoa jahazi siku zijazo au hizi ambazo timu imekuwa ikifanya vibaya.

No comments:

Post a Comment