Saturday, February 25, 2012

Chelsea yazidi kupasua anga England

CHELSEA imeibandua Bolton mabao 3-0 katika mechi ya Ligi Kuu ya England. Alikuwa, Mbrazil, David Luiz aliyefunga bao la kuongoza kwa timu hiyo kabla ya mshambuliaji wa Ivory Coast, Didier Drogba kufunga. Frank Lampard alifunga bao la tatu kwa kumalizia krosi ya Juan Mata.
Mechi nyingine za leo, West Brom iliyokuwa nyumbani iliitandika Sunderland mabao 4-0.
Nayo QPR ilishindwa kutumia uwanja wa nyumbani na kuchapwa bao 1-0 na Fulham wakati Newcastle ikiwa nyumbani ililazimishwa sare ya 2-2 na Wolves. Wigan na Aston Villa zilitoka suluhu.
Drogba

No comments:

Post a Comment