Saturday, February 18, 2012

Simba droo ngoma, Yanga yabanwa Dar

Yanga imeshindwa kutumia uwanja wa nyumbani baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 na Zamalek ya Misri katika mchezo mkali ulipigw akwenye Uwanja wa Taifa.
Yanga iliyokuwa imepania mchezo huo, imejiweka katika mazingira hatari, kwani Zamalek iliyovuliwa ubingwa na Simba 2003, itakuwa ikihitaji ushindi wa bao 1-0 au suluhu waweze kusonga mbele.
Ukiacha hayo ya yanga, Simba nayo imetoka sare ya 1-1 na Kiyovu ya Rwanda katika mchezo mwingine wa Kombe la Shirikisho Afrika.
Yanga kama ilivyo Simba, ilipata bao lake kupitia kwa Hamis Kiiza katika dakika ya 36 wakati lile la Simba lilifungwa na Mwinyi Kazimoto mchezo uliofanyika kwenye Uwanja wa Nyamirambo.
Zamalek ilisawaisha kipindi cha pili kupitia kwa mshambuliaji wake matata Amr Zaki na kuiweza timu yake katika nafasi nzuri ya kusonga mbele wiki mbili zijazo.
Simba nayo inahitaji ushindi ama suluhu ya bila mabao iweze kuingia raundi ya kwanza kwani itakuwa na faida ya bao la ugenini.

No comments:

Post a Comment