Thursday, February 16, 2012

Simba watua Kigali kuwavaa Kiyovu

Okwi, tegemeo SSC
Wachezaji na viongozi wa klabu ya Simba, wamewasili kwenye mji wa Kigali, Rwand tayari kwa mchezo wa kwanza wa raundi ya kwanza wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Kiyovu Sports, mchezo utakaofanyika Jumamosi.
Habari kutoka Kigali zinasema kuwa wachezaji wote wako katika hali nzuri tayari kwa mchezo huo.
Wachezaji walioondoka ni makipa Juma Kaseja na Ali Mustapha 'Barthez'.
Mabeki: Nassor Said 'Cholo', Juma Jabu, Juma Nyoso, Kelvin Yondan, Victor Costa na Obadia Mungusa.
Viungo walioondoka ni Shomari Kapombe, Mwinyi Kazimoto, Jonas Mkude na Patric Mafisango wakati washambuliaji ni Ramadhani Singano 'Messi', Edward Christopher, Salum Machaku na Uhuru Selemani, Felix Sunzu na Emmanuel Okwi.
Viongozi wa timu yumo Makamu Mwenyekiti, Geofrey Nyange 'Kaburu', Katibu mkuu Evodius Mtawala, Fransis Silaya (Mjumbe wa kamati ya utendaji) Ibrahim Masoud, Milovan na msaidizi wake Amatre, Cosmas Kapinga (daktari) na James Kisaka ambae ni kocha wa makipa.

No comments:

Post a Comment